Single Event

TIMU YA CHUO CHA MIPANGO YA MPIRA WA PETE YAICHAPA TIMU YA WCF MASHINDANO SHIMMUTA

Timu ya  Wanawake ya Mpira wa Pete ya Chuo cha Mipango  Jumatano tarehe 15 Novemba , 2023 imeichapa bila huruma timu ya WCF (Workers Compensation Fund) kwa magoli 35 kwa 17 katika Mashindano ya Shirikisho la  Michezo ya Mashirika ya Umma , Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMMUTA) yanayoendelea Jijini Dodoma.

Mchezo mwingine utachezwa hapo kesho majira ya saa 9:50 Alasiri ambapo timu ya IRDP itakutana na  timu ya BOT (Bank Of Tanzania) , mchezo utakaopigwa katika Viwanja vya Kilimani.

Akizungumzia  maandalizi na hali ya Kambi  kuelekea mchezo huo, Mwalimu wa timu  Bw. Mafuru Guriro amesema hali ya Kambi ni nzuri na hakuna majeruhi wowote na kwamba ushindi wa leo umewapa ari kubwa ya kuendelea kushinda.

" Wachezaji wangu wote  wana ari kubwa na nitumie fursa hii kuwatumia salamu timu tutakazo kutana nazo wajiandae kisaikolojia. Kwa upande wa BOT wajiandae kupigwa na kitu kizito kichwani ". Alisema Bwana  Mafuru