Single Event

TIMU YA MPIRA WA PETE YAANZA KWA KUPOTEZA MECHI YAKE YA KWANZA MASHINDANO SHIMMUTA

Timu ya Wanawake ya  Mpira wa Pete ya  Chuo cha Mipango (IRDP) imepoteza mchezo wake wa kwanza  dhidi ya Timu ya Bandari  (TPA)  kwa  kufungwa magoli 46 kwa 15 katika Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Mashirika ya Umma Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania  (SHIMMUTA) yaliyoanza jana Jumapili tarehe 12 Novemba 2023 Jijini Dodoma.

Akizungumza mara baada ya Mchezo huo  uliochezwa katika Viwanja vya Jamhuri Katibu Mkuu wa Mipango Sports Club Dkt. Swaumu Mkomwa alisema kuwa  timu hiyo imepoteza mechi  kutokana na kuwa na muda mchache wa kujiandaa na kufanya mazoezi. Hata hivyo   ameahidi kuwa timu hiyo itafanya vizuri katika mechi zijazo.

" Niwapongeze wachezaji wangu  kwa kucheza vizuri japo  hatukupata matokeo mazuri. Ila tunaahidi kufanya vizuri katika mechi zijazo". Alisema Dkt. Swaumu

Ikumbukwe kuwa Timu  hiyo ya Bandari  ni bingwa mtetezi wa mpira wa Pete wa Mashindano ya Shimmuta mwaka jana 2022.