Single Event

Maonesho ya Vyuo vya Elimu Juu yaliyoandaliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania ( TCU) Julai 2022

Kwenye Maonesho ya Vyuo vya Elimu Juu  yaliyoandaliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania ( TCU) katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam Makamu Mkuu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini  (IRDP) anayeshughulikia Taaluma, Utafiti na Ushauri Elekezi, Profesa Provident Dimoso amesema kuwa chuo hicho kina tatua changamoto za ajira kwani kimeanzisha kituo cha Ubunifu na Ujasiriamali kwa wanafunzi wote wanaosoma katika chuo hicho.

Pia amewakaribisha  wahitimu wa kidato cha nne kwa ajili ya kujiunga na masomo ya ngazi ya cheti na waliomaliza kidato cha sita kujiunga ngazi ya  Shahada 'degree' pamoja na  wale ambao ufaulu wao  ni wa alama moja ' Principal Pass'  nao wanaweza kujiunga na chuo hicho kwa ngazi ya diploma.

" Imekuwa ni utamaduni kwa Watanzania kudhani kwamba ukimaliza kidato cha sita na ukapata alama moja ya ufaulu wanadhani wamefeli mwanafunzi anaweza kuendelea na masomo kwa kusoma masomo ya diploma ya chuo hiki," amesema Prof. Dimoso.

Prof. Dimoso ameongeza  chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini kinatambuliwa na TCU  na kina usajili wa Baraza la elimu na mafunzo ya ufundi (NACTEVET), hivyo mwanafunzi anaposoma Shahada katika chuo hicho uzito wake ni sawa na kusoma chuo chochote duniani kwa kuwa ni kizuri,kina ubora na kimejikita kwenye masuala ya mipango.

KUPANGA NI KUCHAGUA